Home Back

Netanyahu alivunja Baraza lake la Vita

jamhurimedia.co.tz 2024/7/7

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amelivunja Baraza lake la Vita ambalo husimamia operesheni za kijeshi huko Gaza. Mapigano yanaendelea pia kuripotiwa katika ardhi ya Palestina huku idadi ya vifo pia ikiongezeka.

Taarifa ya kuvunjwa kwa baraza hilo la vita la Israel lenye wanachama sita, imetangazwa na msemaji katika ofisi ya waziri mkuu David Mencer. Hatua hii inakuja baada ya kujiondoa kwa mbunge wa upinzani Benny Gantz ambaye kwa wiki kadhaa sasa amekuwa akimlaumu Netanyahu kuwa ameshindwa kuwa na mpango thabiti katika vita vya Gaza.

Maafisa wa serikali ya Israel waliozungumza kwa sharti la kutotajwa majina wamesema kwa sasa Netanyahu ambaye amekuwa akikabiliwa na shinikizo la ndani na hata kimataifa, atakuwa akifanya majadiliano kuhusu vita hivyo na kundi dogo la mawaziri akiwemo waziri wake wa Ulinzi Yoav Gallant.

Mbunge wa upinzani Benny Gantz aliyejiondoa kwenye Baraza la Vita la NetanyahuPicha: ABIR SULTAN/EPA
Kwa miaka mingi Benny Gantz amekuwa mpinzani mkuu wa Netanyahu na alikubali kujiunga na serikali yake kama ishara ya mshikamano baada ya shambulio la Hamas la Oktoba 7 mwaka jana.

Lakini amechukua uamuzi wa kujiondoa akisema haafikiani na maamuzi ya Netanyahu katika vita hivyo. Mara kadhaa Benjamin Netanyahu amekuwa akitaja kuwa hatua zote anazochukua ni kwa manufaa ya taifa la Israel.

People are also reading