FC Lupopo Yataka kuifanyia umafia Yanga Kwa Boka
Klabu ya FC Saint Eloi Lupopo inataka kuifanyia umafia Yanga juu uhamisho wa beki wa kushoto Chadrack Issaka Boka ambaye tayari Wananchi wamemsainisha mkataba wa miaka miwili.
FC Saint Eloi Lupopo wanadai ni mchezaji huyo ni wao na wameiambia Chama cha soka Nchini DRC (FA) kisitume ICT kwenda Yanga kwa ajili ya kukamilisha usajili huo.
Hata hivyo kwa mujibu wa vielelezo ambavyo KitengeTV inavyo, nyota huyo siyo mchezaji wa FC LUPOPO bali ni mchezaji wa Real Of Kinshasa na alijiunga na Fc Lupopo kwa mkopo.