Home Back

Bomet: 2 Wafariki, 4 Wajeruhiwa Magari Yakigongana Katika Barabara Kuu ya Bomet-Kaplong

kiswahili.tuko.co.ke 2024/10/6
  • Watu wawili walifariki kwenye ajali ya kuogofywa kwenye barabara kuu ya Bomet-Kaplong Jumatatu, Juni 10, eneo la Mikingo
  • Kamanda wa polisi kaunti ya Bomet Robinson Ndiwa alithibitisha ajali hiyo ilitokea wakati gari moja lilikuwa likikwepa kugonga gari lililokuwa limesimama
  • Watu waliojeruhiwa walikimbizwa katika Hospitali ya Misheni ya Kaplong, huku ajali hiyo ikisababisha msongamano mkubwa wa magari kwa takriban saa mbili

MAKINIKA: Tufuatilie kwenye Instagram - pata habari muhimu zaidi moja kwa moja kwenye app yako uipendayo!

Bomet - Watu wawili wamethibitishwa kufariki kufuatia ajali kwenye barabara kuu ya Bomet-Kaplong.

Bomet: 2 Wafariki, 4 Wajeruhiwa Magari Yakigongana Katika Barabara Kuu ya Bomet-Kaplong
Kamanda wa polisi kaunti ya Bomet Robinson Ndiwa alisema ajali hiyo ilihusisha magari mawili yaliyogongana. Picha: ABC. Chanzo: UGC

Ajali hiyo ya alasiri ya Jumatatu, Juni 10, ilihusisha magari mawili yaliyogongana kwenye barabara yenye shughuli nyingi katika eneo la Mikingo.

Akithibitisha kisa hicho, kamanda wa polisi kaunti ya Bomet Robinson Ndiwa alisema magari hayo yalikuwa yakielekea upande tofauti.

Kulingana na Citizen Digital, mojawapo ya magari hayo yaliacha njia yake huku dereva wake akijaribu kukwepa kuligonga gari lililokuwa limeegeshwa kwenye ukingo wa barabara.

MAKINIKA: Watumie wahariri wetu taarifa yako unayoiona kuwa bora! Tafadhali wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Wengi wa waliojeruhiwa walikimbizwa katika Hospitali ya Misheni ya Kaplong huku wengine wakinusurika mkono wa maunti.

Magari hayo yalipelekea kutoke kwa msomgamano mkubwa kwa takriban saa mbili huku polisi wakitaka kuhakikisha hali ya kawaida inarejea.

Miili ya marehemu ilipelekwa katika hifadhi ya maiti ya hospitali ya Kapkatet.

Chanzo: TUKO.co.ke

People are also reading