Home Back

Kanoute Afuata Nyayo za Mwamba Clatous Chama , Nae Aondoka Simba

udakuspecially.com 2024/10/5

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa

BAADA ya sakata la Clatous Chama kutopata suluhu hadi sasa, Uongozi wa Simba unakabiliwa na changamoto mpya ya kumshawishi kiungo wake Sadio Kanoute asalie klabuni hapo.

Hivi karibuni, mazungumzo kati ya Simba na Chama kuhusu kuongeza mkataba wake yalishindwa kufanikiwa kwani kuna ripoti kwamba Mzambia huyo tayari amejiunga na Yanga.

Hatua hiyo imewaudhi baadhi ya wanachama na mashabiki wa Simba ambao wanaamini kuwa Chama bado ni muhimu kwa klabu hiyo. Kuna ripoti kwamba nae Sadio Kanouteameomba kuondoka Simba.

Mchezaji huyo wa Mali alijiunga na Simba katika msimu wa 2021/2022 akitokea Al-Ahli Benghazi ya Libya, ambayo ilimnunua kutoka Stade Malien.

Kanoute ameisaidia sana Simba katika mechi za ndani na kimataifa.

Licha ya kucheza katikati ya uwanja, Kanoute ameweza kufunga mabao kadhaa muhimu kwa Simba, na kuwa mmoja wa wachezaji wanaotegemewa.

Hata hivyo, bado hajashinda medali katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la CRDB tangu alipojiunga na Simba.

Hata hivyo, Kanoute anajivunia kushinda medali ya Ngao ya Jamii mwanzoni mwa msimu wa 2023/2024, pamoja na kushinda Ubingwa wa Ligi ya Muungano ulioshirikisha timu nne.

Kulingana na chanzo ndani ya klabu, Kanoute, ambaye bado ana mkataba wa mwaka mmoja, ameomba kuondoka kutafuta changamoto mpya katika kazi yake.

Hata hivyo, suala hilo bado halijapata idhini kutoka kwa uongozi wa klabu, ambao wanaamini kuwa Kanoute bado ana mchango mkubwa kwa timu hiyo, licha ya uamuzi wake hata kama atauzwa kwa timu nyingine.

“Bado kuna suala na Kanoute kubaki Simba. Ameomba kuondoka na amekuwa akisisitiza. Uongozi umezungumza naye, lakini bado amesimama imara kwenye uamuzi wake. Kwa sasa, ni karibu hakika ataondoka, na nafasi za kubaki ni ndogo sana,” kilisema chanzo hicho.

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, alithibitisha kwamba Kanoute ameomba kuondoka, lakini uongozi bado haujaamua kuhusu suala lake.

“Ni kweli tuko kwenye mazungumzo na mchezaji, na anaomba changamoto mpya. Hata hivyo, hakuna makubaliano yaliyofikiwa ikiwa ataondoka au la,” alisema Ally.

_________

LOVE STORY YA UTANIKUMBUKA NEYLA Ipo tayari ni maandishi na Sauti !, Kuisoma yote Bonyeza HAPA Lipia tsh 1000 Tu mtandao wowote,au Tembelea www.makapedia.com

People are also reading