Nairobi: Askari Auawa baada ya Kumpiga Risasi Hakimu Mfawidhi wa Makadara Kortini
MAKINIKA: Tusaidie kubadilisha maisha ya wengi, jiunge na programu ya Patreon kutoka TUKO.co.ke.
Nairobi - Hakimu anauguza majeraha mabaya baada ya kupigwa risasi katika Mahakama ya Makadara jijini Nairobi.
Citizen Digital iliripoti kuwa Hakimu Mkuu Monica Kivuti alipigwa risasi na afisa wa polisi ndani ya chumba cha mahakama kufuatia mabishano.
Kulingana na polisi, amri za korti zilimzima mara moja afisa huyo ndani ya Chumba cha 9.
Uchunguzi wa awali unaonyesha ofisa huyo alikuwa mume wa mshitakiwa ambaye anadaiwa kumfyatulia risasi hakimu huyo baada ya mke wake kufutiwa dhamana kwa kususia kuhudhuria mahakama.
Kimani Ichung'wah Azidi Kumlima Rigathi Gachagua, Asema Hastahili Kabisa Kupewa Helikopta ya Kijeshi
MAKINIKA: Watumie wahariri wetu taarifa yako unayoiona kuwa bora! Tafadhali wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Makachero kutoka idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai walifika katika eneo la tukio kuchunguza kisa hicho.
Maafisa wa Kitengo cha Polisi cha Kupambana na Ugaidi (ATPU) walizingira eneo la uhalifu katika Mahakama ya Makadara, Nairobi huku watoa huduma za dharura wakimkimbiza hakimu hospitalini.
Sababu ya vitendo vya askari huyo bado haijajulikana
Mengi zaidi ya kufuata...
Chanzo: TUKO.co.ke