Home Back

GARI LA POLISI LAUA POLISI 'Trafiki' AKIKAGUA MAGARI BARABARANI

malunde.com 2024/7/7

Polisi wameanzisha uchunguzi baada ya afisa wa trafiki kukanyagwa alipokuwa akitekeleza majukumu yake rasmi katika kaunti ya Bungoma nchini Kenya.

Citizen Digital iliripoti kwamba afisa wa trafiki alifariki papo hapo baada ya kugongwa na gari la polisi eneo la Cheptais Junction Jumapili, Juni 9,2024. 

Ripoti ya polisi inasema kuwa Fredrick Juma, ambaye anahudumu katika kitengo cha Ulinzi wa Miundombinu (CIPU) huko Bungoma Magharibi, alisimamisha trela ya Abdullahi Bunyori kwa ukaguzi wa kawaida. 

Wakati akimhoji dereva huyo, Juma aligongwa na gari aina ya Toyota Land Cruiser kutoka Kituo cha Polisi cha Sirisia, lililokuwa likitokea upande wa pili.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa Gideon Magut, akiendesha gari la polisi, alifanikiwa kukwepa kuligonga lori lililokuwa limeegeshwa kando ya barabara. 

Afisa huyo wa trafiki alifariki papo hapo baada ya kupata majeraha mabaya kichwani. 

"Kutokana na kugongwa, marehemu alitupwa upande wa mbele, akapata majeraha mabaya kichwani na alikufa papo hapo," ripoti ya polisi ilisema kwa sehemu. 

Mwili wa marehemu ulihamishwa hadi katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Life Care ukisubiri uchunguzi wa baada ya maiti.

Chanzo - Tuko news

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
People are also reading